Friday 28 June 2013

Karibuni katika blogu yangu mpya ya kazi za mikono yangu..

Ninamshukuru Mungu kila siku kwa baraka alizonipa katika mikono yangu. Mungu amenibariki kumudu kazi nyingi za sanaa ya mikono inayotawala ikiwa ni ya USHONAJI.

Blogu hii itakuwa ikiwaletea kazi zangu mbalimbali za ushonaji wa vitu mbalimbali kama vile Mavazi, Mapazia, Mashuka, Mapambo ya aina zote na vitu vingine vingi nitakavyokuwa nikiendelea kuvigundua.

Karibuni Mlango uko wazi...!!!

Vitambaa tayari kufanyiwa kazi ya sanaa..

    Kola ya shati la kiume...

Shati likiwa katika hatua za mwisho... Wanaume mmepata suluhisho ninashona nguo zote, za kiume (mashati, suruali, suti na kadhalika..) 

 Hadi wakati mwingine..

 Da' Mija.

4 comments:

  1. Dada mkuu msaidizi hongera na nakutakia kila la kheri.

    ReplyDelete
  2. hongera sana, shati hilo ntalipataje nikiwa Rwanda au Tanzania?

    ReplyDelete
  3. Kakangu Justine, Shati ninatuma popote pale unapokuwa...Tuwasiliane tu.

    Yasinta asante sana dada mkuu..

    ReplyDelete


  4. Biblia Kwenye Mtandao

    BIBLIA TAKATIFU--TAFSIRI YA ULIMWENGU MPYA
    Methali 31:1-31
    =========================================================
    Maneno ya Lemueli mfalme, ujumbe mzito+ ambao mama yake alimwambia ili kumrekebisha:+ 2 Niseme nini, ewe mwanangu, niseme nini, ewe mwana wa tumbo langu,+ niseme nini, ewe mwana wa nadhiri zangu?+ 3 Usiwape wanawake nguvu zako za uhai,+ wala njia zako kwa kitu ambacho hufanya wafalme wafutiliwe mbali.+ 4 Haifai wafalme, ewe Lemueli, haifai wafalme kunywa divai wala maofisa wakuu kuuliza: “Kileo kiko wapi?”+ 5 ili mtu asinywe na kusahau jambo lililoagizwa na kupotosha haki ya yeyote wa wana wa mateso.+ 6 Mpeni kileo mtu yeyote anayekaribia kuangamia+ na kuwapa divai watu wenye uchungu katika nafsi.+ 7 Acheni mtu anywe na kuusahau umaskini wake, na mtu asiikumbuke taabu yake tena. 8 Fungua kinywa chako kwa ajili ya mtu asiyeweza kusema,+ ili kutetea watu wote wanaopitilia mbali.+ 9 Fungua kinywa chako, hukumu kwa uadilifu na kutetea mtu mwenye kuteseka na maskini.+ א [ʼA′leph] 10 Mke mwenye uwezo, ni nani anayeweza kumpata?+ Thamani yake inapita sana ile ya marijani. ב [Behth] 11 Moyo wa mume wake umemtegemea, wala hakuna faida inayokosekana.+ ג [Gi′mel] 12 Amemthawabisha mume wake kwa mema, wala si kwa mabaya, siku zote za maisha yake.+ ד [Da′leth] 13 Ametafuta sufu na kitani, naye hufanya kazi yoyote inayopendeza mikono yake.+ ה [Heʼ] 14 Amekuwa kama meli za mfanyabiashara.+ Huleta chakula chake kutoka mbali. ו [Waw] 15 Tena huamka kabla usiku haujaisha,+ na kuwapa watu wa nyumbani mwake chakula na kuwapa vijana wake wa kike fungu lao lililoamriwa.+ ז [Za′yin] 16 Amefikiria shamba, akalinunua;+ amepanda shamba la mizabibu kutokana na matunda ya mikono yake.+ ח [Chehth] 17 Amejifunga nguvu viunoni, naye ameitia nguvu mikono yake.+ ט [Tehth] 18 Ametambua kwamba biashara yake ni nzuri; taa yake haizimiki usiku.+ י [Yohdh] 19 Amenyoosha mikono yake kushika kijiti cha kusokotea uzi, nayo mikono yake mwenyewe imeshika gurudumu la kusokota nyuzi.+ כ [Kaph] 20 Amewanyooshea mkono wenye kuteseka, na mikono yake amemkunjulia maskini.+ ל [La′medh] 21 Hana wasiwasi juu ya watu wa nyumbani mwake kwa sababu ya theluji, kwa maana watu wote wa nyumbani mwake wamevaa mavazi mawili.+ מ [Mem] 22 Amejitengenezea matandiko yenye mapambo.+ Mavazi yake ni ya kitani na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau.+ נ [Nun] 23 Mume wake+ ni mtu anayejulikana malangoni,+ anapoketi pamoja na wanaume wazee wa nchi. ס [Sa′mekh] 24 Hata ametengeneza mavazi ya ndani+ na kuyauza, nao wafanya-biashara amewapa mishipi. ע [ʽA′yin] 25 Nguvu na fahari ndiyo mavazi yake,+ naye anaucheka wakati ujao.+ פ [Peʼ] 26 Hufungua kinywa chake kwa hekima,+ na sheria ya fadhili zenye upendo ziko katika ulimi wake.+ צ [Tsa·dheh′] 27 Anaangalia shughuli za nyumba yake, wala hali mkate wa uvivu.+ ק [Qohph] 28 Wanawe wamesimama na kumtangaza kuwa mwenye furaha,+ mume wake husimama, naye humsifu.+ ר [Rehsh] 29 Kuna binti wengi+ ambao wameonyesha uwezo, lakini wewe—wewe umewapita hao wote.+ ש [Shin] 30 Uvutio unaweza kudanganya,+ nayo sura yenye kupendeza inaweza kuwa ubatili;+ lakini mwanamke anayemwogopa Yehova ndiye anayejiletea sifa.+ ת [Taw] 31 Mpeni baadhi ya matunda ya mikono yake,+ nazo kazi zake na zimsifu malangoni.+ {Chanzo:www.jw.org/sw}

    ReplyDelete